Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (#CCM) Taifa imetangaza mabadiliko katika safu yake ya Uongozi, ambapo imemteua Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Kenani Kihongosi kuwa Katibu wa Itikadi, Uenezi na Mafunzo wa CCM, nafasi iliyokuwa ikishikiliwa na Amos Makalla ambaye ameteuliwa na Rais Samia kuwa Mkuu wa Mkoa wa Arusha.
Aidha, Dkt. Asha-Rose Migiro ameteuliwa kuwa Katibu Mkuu wa CCM akichukua nafasi ya Dkt. Emmanuel John Nchimbi ambaye chama kimempitisha kuwa Mgombea Mwenza wa Dkt. Samia Suluhu katika Uchaguzi Mkuu wa 2025.
